FREEMASON NA MUUNGANO WA MAKANISA



Ili kufanikiwa katika malengo yao ya kuitawala dunia kupitia Dini, uchumi, siasa na
Ajira/kazi, Illuminati walifanikiwa kuanzisha taasisi za Kidini, kiuchumi, kisiasa na kazi na ajira, zote hizo zikiwa zinafanya kazi kwa mwongozo wa Illuminati. 

Katika taasisi za kidini tunakuta Baraza la Umoja wa makanisa ulimwenguni (World Council of Churches) ambalo lilianzishwa na Illuminati kwa makusudi ya kuunganisha dini zote za Kikristo na kutengeneza “Mnara wa Babeli” wa kiroho.

[​IMG]

Tayari kuna makanisa mengi ambayo yamejiunga kwenye umoja huo. Wengi hawajui kama umoja huo uko chini ya chama cha siri cha Illuminati ambacho kina siri kubwa sana katika kutawala dini na dunia kwa ujumla.

Ukitaka kujua kama kanisa lako ni mwanachama wa Baraza hilo unaweza
kutembelea mtandao wa Baraza hilo kwenye

http//www.wcc-coe.org/.

Ieleweke kwamba WCC ina vitengo kama Christian World Communion, Global Christian Forum, nk. ambapo kanisa linaweza lisiwe member wa WCC moja kwa moja ila likawa member wa vitengo vilivyo chini ya WCC.

Siri ambazo Illuminati/Freemason hawataki zifahamike kwa watu Kuna siri muhimu ambazo Freemason na Illuminati hawataki zifahamike kwa watu. Siri hizo ni:

– Viongozi wa dini wamefanikiwa kuwatawala mamilioni ya wanaume na
wanawake, ambao wamekuwa wakifundishwa tangu utoto wao, kwamba viongozi
hao ni wajumbe kutoka kwa Mungu.

– Leo viongozi hao wamezungukwa na mamia ya alama na mavazi ya Freemason
kama vile pete, kofia nk kiasi kwamba watu wengi hawajui hilo.

[​IMG]

[​IMG]

– Illuminati wanaamini kwamba kuna zaidi ya Mwokozi mmoja aliyesulubiwa.
Kwamba wapo zaidi ya ishirini.

– Illuminati wanaamini kwamba Yesu alifundishwa na waalimu kutoka Misri.

– Kisha Yesu akawa “jua” na wale wanafunzi wake kumi na wawili wakawa ndio ishara kumi na mbili zinazotumiwa na Freemason zinazozojulikana kama Zodiac
[​IMG]

– Mbingu zinasemekana kuwa ziko “juu” hata hivyo kutokana na mzunguko wa dunia (rotation of the Earth) juu na chini hubadilishana mahali pake.

– Wanaoingia kwenye vyama hivi vya siri huanza kupanda ngazi (uti wa mgongo)
hadi juu kwenye kilele cha mlima (ubongo), wakiwa wanapitia kwenye shimo
lililoko sakafuni. Mahali hapo ndipo palipo na hekima (wisdom).

– Utatu (trinity au triune) katika mwanadamu ni moyo, ubongo, na viungo vya siri –
kila kimoja kimepewa kiwakilishi cha alama katika degree tatu za kwanza za Freemason.

Moyo na ubongo huitwa Kaini na Habili. Vyote viwili vinawajibika kuleta usawa kamili (total equilibrium).

– Mti uitwao Pine wenye majani yenye ncha kama sindano ni sawa na mkia wa nyoka wenye kitu kama kidole kinachoitwa mkuki mtakatifu. Hiki ndicho
kinachounganisha mambo ya zamani na yaliyopo (old and present)

– Uti wa mgongo ni sawa na nguzo yenye ngazi 33 ambazo wakati mwingine huitwa nyoka au wachawi.

Hii ndio fimbo ya Her-me ikiwa imezungukwa na nyoka wawili, mmoja mweusi mwingine mweupe. 

[​IMG]

Na ndio maana ya degree 33 za
Freemason.
– Kiungo kati ya ubongo na viungo vya siri mwilini kinatokana na uti wa mgongo
ambao ndicho kiungo chao – yaani ubongo na viungo vya siri huunganishwa na uti wa mgongo wenye ngazi 33.

– Freemason wanafundisha kwamba mtawala wao ambaye wanamwita mungu anajulikana kwa watu wote kama “Mimi niko”

– Freemason wa kiwango cha juu kabisa wanaamini kwamba watu wengi ni wazito
kama mawe, wakiwa wanafaa kutumiwa kwenye ujenzi kama matofali, uzito wao unatokana na ugumu wao wa kuamini kwamba maana halisi ya maisha ni kuwa na nguvu za kutoa uhai ulimwengunin (giving life in the world).

– Ini (Liver) ndio ufunguo wa damu mwilini. Jina Lucifa ni jina lenye moto,
lisilofanya kazi, sawa na damu isiyo na kazi. Mtu akiwa na ini ni sawa na kusema kwamba anaishi (To have a liver is to live). Neno “Live” ukiligeuza nyuma linakuwa “Evil” yaani uovu na neno “Lived” ukiligeuza linakuwa “Devil” yaani Mwovu. 

Red (Roth) yaani rangi nyekundu ni rangi ya vita. Yellow (Gold) yaani rangi ya njano au ya dhahabu ni ishara ya kupata nguvu, wakati Blue ni rangi
waliyopewa watawala. 

Green (Yellow+Blue) yaani rangi ya kijani ambayo ni mchanganyiko wa rangi ya Blue na njano ni rangi waliyopewa wanaojiunga
kwenye chama cha Freemason (Greenland).

Rangi nyeupe (White) humaanisha silaha, wakati rangi nyeusi ni ishara ya uchawi wa watu weusi (Black Magic)

– Bahari (Meru-Mara-Mary) alikuwa ni bikira mama. Uhai wa kwanza (ndani ya bahari) ulitoka kwenye mdomo wa

1) samaki na kisha kutokea kwenye ardhi kupitia

2)chura. baadae uhai ukapatikana kutoka kwa

3)nguruwe pori dume, kisha
4)simba na hatimaye

5)nyani. Kisha uhai ukabadilika na kuonekana kuwa

6)mtu(hatua ya sita). Tumbo lililoleta mabadiliko haya ya uzazi ni Bustani ya Edeni na
huwakilishwa na herufi “O”. Kisha mtu akavumbua moto (Lumerian #

7) huko Ethiopia wakiwa ni watu wafugaji. Walivumbua pia bahari ya Atlantic (The Atlanteans #

8) wakati wakifuatilia jua lilipokuwa linazama upande wa
magharibi. Mwisho, watu walioitwa (Aryans #

9) walionekana kwa mara ya
kwanza huko Georgia kwenye milima ya Caucuses. Hivyo Freemason wakaamini
kwamba uumbaji haukukamilika na wao wakawa “miungu.”

– Watu hawa waitwao Aryans wanapatikana kwenye kitabu cha Mwanzo sura ya 2
katika Biblia. Wakiwa wanatumia genes zenye umbo la pembe tatu walianza kazi
ya “New World Order”, wakiwafanya watu wazaliane kama nyuki kwenye
mzinga, wakati nyuki wa kiume hugeuka na kisha kuanza kuzaa bila msaada wa nyuki wa kike. (Adamu alitolewa ubavu na mahali pake pakawekwa yai
lililotolewa kwenye test – tube.

Baada ya miezi tisa, akazaliwa mtoto mwanamume aitwaye Tubal Cain, na hatimaye akapelekwa huko Babeli.

Hivyo Freemason wakaanzisha mapango wao na kuuona wenye mafanikio kama ya nyuki.

– Freemason wanasema kwamba mtu mpya hazaliwi mara moja. Wanasema
kwamba mtu huzaliwa kwa degree. Wakati wa miezi tisa mtu huzaliwa akiwa njiti
(pre-mature). Mtu huyo anahitaji kutengenezwa zaidi.

Freemason wanasema kwamba utambuzi wa kiroho “Spritual consciousness” ni “mimi niko” wa kweli, ambaye hupatikana baada ya mwaka wa ishirini na moja wakati mawazo huanza kutoka katika viungo wa siri (kukomaa kwa balehe). Hata hivyo kwa Freemason maisha huanza mtu anapofikisha umri wa miaka arobaini, baada ya miaka ishirini ya kujitoa kwake, na kuwa mtumishi mwaminifu.

– Wanawake, hamuoni kwamba mnapaswa kuamka na kuwatuma freemason wa
kike kwenye vikao.

Mkiendelea kukubali kunyanyaswa kiakili, kimwili na kiroho nguvu zetu zitakwisha. Msikubali kuendelea kunyanyaswa.

Jiteteeni katika maisha yenu na taratibu ulimwengu wote utafadhaika.

– Kwamba kanisa au dhehebu lazima liwe chini ya uongozi wa watu katika mfumo wa umbo la pembe tatu (Piramidi) na kwamba mtu hawezi kuokolewa asipokuwa ndani ya kanisa au dhehebu hilo.

– Baada ya miaka elfu kumi ya Freemason, je huu sio wakati wa wanaume na wanawake kujichukulia madaraka ya kisiasa, kidini na kiuchumi na kuunda paradiso ambayo ilikuwa imepotea hapa duniani?

Hizo ndizo baadhi ya siri muhimu ambazo Freemason hawataki zijulikane kwa watu.

Ukichunguza kwa makini siri hizo utagundua mambo mengi ikiwa ni pamoja na maana ya degree 33. Lakini pia utagundua kwamba katika somo la Historia kuna topic inayosema “Evolution of man” Yaani uibukaji wa mwanadamu. Kwamba mtu hakuumbwa kama Biblia inavyosema ila alitokana na mabadiliko ya viumbe kutoka hatua ya kwanza hadi ya 9.

Sasa ieleweke kwamba chanzo cha topic hiyo ni Freemason. Jambo lingine ni kwamba siku za hivi karibuni wanasayansi wamekuwa wakifanya utafiti wa
kuzalisha watoto kupitia chupa (Test Tube). Hiyo pia ni imani ya Freemason ambao wanaamini kwamba Adamu alipotolewa ubavu, kama Biblia inavyosema, wanadai aliwekewa yai kupitia kwenye chupa (test tube) na kisha akazaliwa Tubal Cain bila
msaada wa mwanamke. 

Wao wanasema bahari ndio mwanamke na tutaona katika mada za mbeleni kwenye jinsi freemason wanavyopata nguvu kutoka kwa jinni liitwalo LILITH ili kuwaweka wanawake mahali ambapo hawakuwekwa na Mungu.

Ndio maana tunaona harakati za kuwanyanyua wanawake ili washike majukumu ya wanaume, hata hivyo Freemason wanajua kwamba hilo litakapofanikiwa,ulimwengu
wote utafadhaika!

Lakini pia Freemason wanasema kwamba watu wana mioyo mizito kwa sababu hawawaamini na hivyo wamekuwa wazito kama mawe ambayo yanafaa kutumiwa katika ujenzi. Hivyo wanawatumia watu kujenga babeli yao bila watu kujua.

Kwa mfano watu wengi wamekuwa wakiiga mitindo ya kidunia iliyoanzishwa na
Freemason, madhehebu mengi yamekuwa yakifuata mafundisho yaliyo maagizo ya
wanadamu (Mathayo 15:9), madhehebu mengi yamefuata mfumo wa Piramidi, na kwa
kweli wengi wamekuwa ni mawe mazito yanayotumiwa na Freemason kujengea.

FREEMASON NA KAZI ZAO

Sasa tunaingia katika hatua muhimu kabisa ya kujua kazi za vyama hivi vya siri maana tayari vimo ndani ya jamii bila jamii yenyewe kujua.

Tumeona mnyama wa
namba 666(PAPACY SYSTEM) na Illuminati, ambao malengo yao ni mamoja, ya kuitawala dunia, kisiasa, kiuchumi, kidini nk.

Ukweli ni kwamba huwezi kutenganisha Illuminati na Freemason .

Lakini pia huwezi kuwazungumzia freemason bila kumfahamu na kumtaja Dr.Albert Pike.

Dr. Albert Pike alizaliwa Disemba 29, 1809 akiwa ndiye mtoto mkubwa kwenye
familia ya watoto sita ya Benjamin na Sarah Andrews Pike. Pike alizaliwa na kukulia kwenye familia ya Kikristo kwenye dhehebu la Episcopal. Akiwa na umri wa miaka 15 alifanya mtihani wa Harvard College na akafaulu lakini hakuweza kusoma chuoni hapo kwa sababu ya kukosa fedha. Baada ya kusafiri hadi kufika mahali panapoitwa Santa, aliendelea na safari yake hadi Arkansas ambapo aliajiriwa kuwa mhariri wa gazeti kabla ya kufanya kazi bar. Akiwa Arkansas, alikutana na Mary Ann Hamilton na akamuoa Novemba 28, 1834. Aliweza kuzaa watoto 11 pamoja na mkewe. 

Alipofikisha umri wa miaka 41 aliomba kujiunga na freemason kwenye Loji inayoitwa Western Star Lodge No. 2 huko Little Rock, Ark ikiwa ni mwaka 1850. Alipata Digrii zake 10 za York Rite kuanzia mwaka 1850 hadi 1853. Alipata digrii ya 29 ya Scottish Rite mwezi Machi 1853 akiwa Loji ya Albert Gallatin Mackey huko Charleston.

Kwa mujibu wa maandishi ya mwanzo kabisa kuhusu Freemasons, maandishi hayo
yanasema kwamba chanzo cha freemasons ni Adam anayesemekana kuwa ndiye Mason wa kwanza kabisa. Kitambaa kinachoitwa ‘apron’ wanachokivaa Masons wakati wa ibada zao wanadai kuwa ni sawa na ngozi aliyoivaa Adamu na Hawa katika bustani ya Eden. 

Ujuzi wa kujua mema na mabaya alioupata Adamu baada ya kula tunda walilokatazwa ulichukuliwa hadi kwa mtoto wa Adam aitwaye Seth, na kisha kwa Nimrod ambaye ndiye mwanzilishi wa ujenzi wa mnara wa Babeli, yeye akiwa ni kitukuu wa Nuhu. Dr. Albert Mackey (mwenye digrii 33 na mwandishi wa Freemasonry Encyclopedia) anarejea kwenye maandishi ya mwaka 1560 yakielezea kwamba chanzo cha freemasons ni kwenye mnara wa Babeli na kwamba Nimrodi aliwafundisha wajenzi wa mnara huo imani ya freemasons.

Baada ya Mungu kuchafua lugha yao, siri zote za freemasons inasemekana kuwa zilipotea. Wakati mfalme Sulemani (Solomon) alipokuwa anajenga hekalu, freemasons wanaamini kwamba imani yao ilianzishwa tena. Mackey anasema kwamba Sulemani (Solomon) ndiye aliyekuwa Grand Master wao mkuu na Loji (Lodges) zote zilianzishwa na Sulemani.

Hata hivyo Martin L. Wagner ambaye ni muumini wa freemason anafundisha kwamba jina ‘Solomon’ sio jina la kabila ya Israeli kwa sababu maana ya jina hilo yaani Sol-om-on humaanisha jua katika lugha ya kilatini ‘Sol’, katika lugha ya
kihindi ‘om’ na katika lugha ya Misri ‘on’ hivyo kumaanisha kwamba Solomon ndiye mungu jua na mkuu wa Freemasons baada ya Nimrod.

Wakati wa utawala wa Uyunani (Greece) kulikuwa na vikundi vilivyoitwa ‘guilds’ sawa na vyama au ‘unions’ kwa wakati wetu huu. Vikundi kama hivyo viliitwa “Dionysiacs,” huko Roma na ndivyo vilivyohusika na ujenzi wa viwanja vya michezo (stadiums).

Baadae vikundi hivi ndivyo vilivyohusika na ujenzi wa makanisa (cathedrals) na majengo makubwa na baadaye vikapewa majina kama Carpenta, builders, draftsmen, craftsmen katika fani ya ujenzi. Watu hao kulingana na fani zao walikaa kwenye vikundi pamoja na mahali hapo pakaitwa Loji au Lodge. 

Ndio chanzo cha majengo ya kuabudu ya freemasons kuitwa ‘Lodges’. Wale wote waliokuwa na fani ya ujenzi wa majengo waliitwa ‘Masons’ lakini iwapo mtu asiye na ujuzi wa ujenzi wa majengo huku akitaka kujiunga na chama hicho aliitwa ‘Accepted Mason’. Baadae Dr. Albert Pike aliandika kitabu kinachoitwa ‘Morals and Dogma of the Ancient and Accepted Scottish Rite of Masonry’ alichokiandika mwaka 1871. Kitabu hicho ndicho chenye mafundisho na
mwongozo wa imani ya freemasons.

Ndani ya kitabu hicho kuna jumla ya digrii 33 za freemason na walitumia mahesabu katika kutoa digrii zao 33, unadhani waliamua tu? hapana! Walipata digrii 33 kutokana na kinachoaminiwa “human trinity” yaani ‘utatu wa kibinadamu’ kwamba ni moyo, ubongo na viungo vya siri. Wakasema kwamba viungo vya siri na ubongo vinaunganishwa na ngazi 33 za vipingili vya viungo vya uti wa mgongo (joints).

Kwamba uti wa mgongo una ngazi 33 kutoka unapoanzia kwenye viungo vya siri hadi kichwani kwenye ubongo.

Hapa inabidi tuwaulize madaktari watupe ukweli kuhusu hizo ngazi 33 za uti wa mgongo. Mtu anapobalehe ndipo anapoanza kupanda ngazi na anapofikia umri wa kuwa na akili (ubongo) timamu iliyotulia huwa amefikia ngazi ya
juu kabisa katika ubongo, sawa na kumaliza ngazi zote 33 za uti wa ubongo.

Digrii hizo 33 ni kama ifuatavyo: The Blue Lodge (Symbolic.Lodge of Hatimaye
imani ya freemasonry ilisambaa taratibu katika maeneo mengi duniania:

Ufaransa (1718-25) , Ireland (1725-26), Hispania (1726-27), Uholanzi (1731), Ujerumani (1730-33),Africa (1735), Scotland (1736), Ureno (1736), Switzerland (1737), Italia(1733-37), Russia (1731-40), Canada (1745), Sweden (1735-48), Prussia (1738-40), Austria (1742), Poland (1784), na Mexico (1825).

Ili kujiunga na imani hii lazima mtu awe na umri wa miaka 21 (3×7) na kama ni mtoto wa freemason anaweza kujiunga akiwa na umri wa miaka 18 (9+9).

Zipo Loji kuu (Grand Lodges) 150 duniani na kuna wanachama wasiopungua 6,000,000 duniani kote. Kila digrii ina mafundisho yake ambapo kadri freemason anavyopanda ngazi kutoka digrii ya chini kwenda digrii ya juu anafunuliwa siri zaidi kuhusu malengo, ibada na utaratibu mzima wa freemason na Illuminati.

Albert Pike anasema: “The Blue Degrees (the Blue Lodge degrees) are but the outer court or portico of the Temple. Part of the symbols are displayed there to the Initiate, but he is intentionally mislead by false interpretations. It is not intended that he shall understand them; but it is intended that he shall imagine he understand them”. [Albert Pike, Morals and Dogma, p. 819; Emphasis added].

Akimaanisha kwamba

freemason wa digrii za chini hawapaswi kujua siri na maana halisi ya alama za freemason ila huwa anadanganywa ili afikiri kwamba anazijua.

Unaweza kuona aina za digrii hizo; kwa mfano digrii ya 18 inayoitwa ‘Knight of Rose Croix’ hushughulika na elimu ya aina za misalaba na jinsi ya kufanisha kuziingiza ndani ya taasisi na madhehebu mbalimbali kwa imani ya Illuminati na freemason na kwa kweli freemason wa digrii hiyo wamefanikiwa kwa kiwango cha juu kabisa kuingiza aina nyingizi za misalaba ndani ya makanisa na taasisi bila ya waumini kujua maana ya misalaba hiyo. 

Tutaona kwenye sura za mbele katika kitabu hiki. Yapata Januari 22, 1870 Pike alipata maono ya nuru “illuminated” kutoka kwa GAOTU—Shetani—kuhusu mpango maalumu wa jinsi ya kutimiza malengo ya New World Order yaliyowekwa na Adam Weishaupt, miaka 94=9+4=13 au 9×4=36 iliyopita, tangu Mei Mosi, 1776, Malengo hayo yalipangwa yakamilike ifikapo Millenia ya 7.

Ndipo akaanza kwa kuandika kitabu mashuhuri kwa freemason kinachoitwa “Morals and Dogma” ambacho kilichapwa kwa mara ya kwanza mwaka 1871, mwaka mmoja tu baada ya kupokea njozi ya kutekeleza mpango mpya wa dunia. 

Unaweza kujiuliza kwamba hivi mpango wa zamani wa dunia ulikuwa ni upi hadi waweke mpango mpya wa dunia? Freemason wanauita Ukristo kuwa ni “Mpango wa Zamani wa dunia” na hivyo walidhamiria kuharibu Ukristo na hivyo kuanzisha mpango mpya wa dunia (New World Order) ambao ni Upagani. 

Tayari viongozi wakuu wa mataifa ya dunia (UN) wamekuwa wakikutana mjini New York ili kuangalia malengo ya Millenia yamefikia wapi, na kwa uwazi wamekuwa wakisema kwamba kuna umuhimu wa kuharakisha New World Order kwa visingizio vya umaskini, maradhi na ujinga.

Ni njozi gani aliyoipata Pike mwaka 1870?

2 comments:

  1. Vyema sana mwandishi nimesoma ivi toka miaka ya pike mpaka leo kuna usalama

    ReplyDelete
  2. Usiombe ukutwa na utawala wa hawa Jamaa! Cz kukufuru ni lazima

    ReplyDelete

Powered by Blogger.